KIFAFA CHA MIMBA – PREECLAMPSIA, ECLAMPSIA.
Kifafa cha
mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure)
wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile
figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya
ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito).
Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata
wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya
ujauzito.
Ugonjwa wa
kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye
tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza
kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo
hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika
kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo
hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni.
Kutokana
na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto walio tumboni,
inashauriwa kila mjamzito awe anahudhuria clinic na kupimwa msukumo wa damu
(blood pressure) na mkojo ili kuhakikisha kuwa yuko salama.
Iwapo kipimo cha msukumo wa damu ni kikubwa kuliko 140/90 mmHg, ni muhimu kurudia kipimo hicho baada ya muda na kufanya vipimo vingine vya maabara vinavyoweza kujulisha uwepo wa kifafa cha mimba.
Iwapo kipimo cha msukumo wa damu ni kikubwa kuliko 140/90 mmHg, ni muhimu kurudia kipimo hicho baada ya muda na kufanya vipimo vingine vya maabara vinavyoweza kujulisha uwepo wa kifafa cha mimba.
Kwa kawaida ugonjwa huu huwepo kwa
muda fulani bila mjamzito kuona dalili zozote. Ghafla mjamzito anaweza kuanza
kuona dalili kama maumivu ya tumbo juu ya kitovu, kutapika, macho kutokuona
vizuri, kuumwa kichwa, mkojo kuwa na rangi tofauti na kawaida, kupumua kwa
shida, uchovu na maumivu ya viungo au kupoteza fahamu na “degedege“.
No comments:
Post a Comment