Friday, 3 June 2016

CHUMVI HUONDOA MADINI KWENYE CHAKULA



Chumvi- ni kiharibu madini:  kama sukari ni sumu tamu, chumvi inazingatiwa ama kiharibu madini. Matumizi ya chumvi kupindukia yanasababisha figo kuwa dhaifu na hatimae kushindwa kufanya kazi zake.
Ni ukweli usiopingika kuwa chumvi ni muhimu kwa ajili ya radha, lakini matumizi yake ya kupindukia yanaleta madhara mwilini. Watu wengi wanaamini kuwa hawawezi kupika pasipokuwa na chumvi, ndio maana ni vigumu kula pasipo chumvi. Kwa mujibu wa walaji, chumvi sio muhimu kwa maisha na afya pia. Kwa maneno mengine  naweza sema hakuna maendeleo ya mwilini yanayotegemea chumvi.
Mwili wa mwanadamui unahitaji mbegu mbili za chumvi(50grams) kwa sikuambayo tunaipata kupitia mboga. Mlo tunaopata kutokana na matunda na mboga unatupatia chumvi ya asili na hauna hitaji la kuongeza chumvi ya ziada.
Chumvi inamadhara makubwa kiliko faida, mfanyakazi anaweza akahitaji chumvi kufidia ile iliyopotea kwa pumzi. Kama asipoweka chumvi anaweza kupata maumivu  ya mwili, misuli kubana na uchovu.
Kuondoa kabisa matumizi ya chumvi katika mlo itakuwa tiba ya kusinzia na kukoroma. Mtu anahangaika na shinikizo la juu la damu atasaidika kama atapunguza matumizi ya chumvi katika mlo wetu, afya zetu zitakuwa safi. Kwa upande mwingine, matumizi makubwa ya chumvi  yatatupatia maradhi/magonjwa.

No comments:

Post a Comment